Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Asia Pasifiki

Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu Volker Türk atembelea Hospitali ya Nitol, Bangladesh, ambapo baadhi ya wanafunzi walipiga risasi walipokuwa wakishiriki maandamano. (Maktaba)
© UNOHCHR/Anthony Headley

Bangladesh: Ripoti yabainisha ushiriki wa viongozi wa juu katika ukandamizaji

Ukandamizaji wa maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Bangladesh mwaka jana hadi kusababisha kuangushwa kwa serikali  ya muda mrefu ya Waziri Sheikh Hasina ulisababisha vifo vya watu wapatao 1,400 ndani ya siku 46 pekee, wengi wao wakipigwa risasi na vikosi vya usalama, amesema hii leo Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu, Volker Türk, akinukuu ripoti ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, OHCHR.

Sauti
1'58"
Suhaila, msichana mkimbizi kutoka Afghanistan ambaye anaendelea na elimu Kyrgyzstan.
UNHCR

Safari yangu Kyrgyzstan ilikuwa ya matumaini na elimu: Mkimbizi Suhaila

Tukiwa bado katika siku ya Elimu duniani kutana na Suhaila msichana mkimbizi kutoka Afghanistan ambaye kupitia mpango wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi  UNHCR wa kuwahamishia wakimbizi katika nchi ya tatu aliwasili Jamhuri ya Kyrgyzstan ambako sio tu alipata maskani ya kudumu na wazazi wake bali pia matumaini na elimu iliyompa ari ya kurejesha matunda yake nyumbani alikotoka.

Sauti
2'13"
Mradi wa kuimarisha stadi na kufungua fursa za kiuchumi, ISEC miongoni mwa wanawake na vijana, umewezesha wasichana Cox’s Bazaar nchini Bangladesh.
ILO

Sikufahamu ufundi bomba ni nini, sasa ILO imeniwezesha – Msichana Bangladesh

Nchini Bangladesh, mradi wa kuimarisha stadi na kufungua fursa za kiuchumi, ISEC miongoni mwa wanawake na vijana, umewezesha wasichana kuvunja mwiko na kuingia kwenye tasnia ambazo zimezoeleka kuwa ni za wanaume, mathalani ufundi bomba. Mradi huo unaolenga wanufaika 24,000 wenye umri kati ya miaka 18 na 35 unatekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la Kazi duniani, ILO kwa kushirikiana na serikali ya Bangladesh.

Sauti
1'40"