Baraza la Usalama la UN yaitaka Rwanda iache kusaidia waasi wa M23 nchini DRC
- Rwanda yatakiwa iache kusaidia M23
- Yatakiwa pia iondoe jeshi lake DRC
- Rwanda na DRC zianze mazungumzo ya kidiplomasia bila masharti yoyote
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR limetoa ombi la dola milioni 40.4 ili kujiandaa na kutoa huduma za kuokoa maisha na usaidizi kwa wakimbizi wa ndani na waliokimbilia nchi jirani baada ya wakati huu ambapo mashambulizi ya waasi wa M23 yanazidi kufurusha raia
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani WFP, limerejelea kwa kiasi usambazaji wa misaada ya chakula katika sehemu za Goma, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), likitoa msaada muhimu wa lishe kwa wastani wa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miezi 59 waliokumbwa na utapiamlo, huku mapigano ya wiki tatu yakizidi kuathiri vibaya upatikanaji wa chakula kwa wale walio hatarini.
Katika mji wa Ramogi, Mukambo jimboni Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), wanahabari wanaonekana wakiongoza juhudi za kuodoa taka ya plastiki na taka zingine kutoka mifereji ya sokoni.
Wakati waasi wa M23 ikiendelea kusonga mbele kuelekea ‘maeneo mengine ya kimkakati’ mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, baada ya kuteka miji ya Goma jimboni Kivu Kaskazini na Bukavu na Kamanyola jimboni Kivu Kusini Umoja Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu athari mbaya za kutoroka kwa wafungwa kulikoshuhudiwa Goma, pamoja na magereza makuu ya Kabare na Bukavu.
Watoto katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wanakabiliwa na janga lisilo na kifani, wakivumilia ukiukwaji mkubwa wa haki zao, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kiholela, ukatili wa kingono, uandikishaji wa kulazimishwa na utekaji nyara unaofanywa na pande zinazohusika katika mzozo, Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Mtoto imeonya leo jijini Geneva, Uswisi.
Historia ya ulinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa inaonesha ulianza miaka mitatu tu baada ya kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa wenyewe. Na kutokana na umuhimu wa ulinzi wa amani kote duniani, shughuli hiyo imedumu kwa miaka yote hiyo 77 hadi sasa na bado ni muhimu lakini inaendelea kukumbwa na changamoto.