Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Afya

Wanawake mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini wakibeba chakula kilichowasilishwa na  Umoja wa Mataifa na wadau wake.
WFP

WFP yatahadharisha kuhusu tishio la njaa Mashariki mwa DRC  huku watu zaidi wakizikimbia kambi

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani WFP, limerejelea kwa kiasi usambazaji wa misaada ya chakula katika sehemu za Goma, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), likitoa msaada muhimu wa lishe kwa wastani wa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miezi 59 waliokumbwa na utapiamlo, huku mapigano ya wiki tatu yakizidi kuathiri vibaya upatikanaji wa chakula kwa wale walio hatarini.

Mwanafunzi akipatiwa chanjo dhidi ya HPV katika kituo cha afya kusini magharibi mwa Côte d'Ivoire.
© UNICEF/Frank Dejongh

Fahamu mambo 5 kuhusu chanjo ya HPV na saratani ya shingo ya kizazi

  • HPV ni kifupi cha Human Papilloma Virus ambayo ni chanjo dhidi ya saratani  ya shingo ya kizazi.
  • Ina nafasi muhimu katika kutokomeza ugonjwa huu unaoathiri mamilioni ya wasichana na wanawake.
  • Katika kila dakika 2, mwanamke mmoja anakufa kutokana na saratani ya shingo ya kizazi.
  • Kuna baadhi ya maeneo idadi ya wagonjwa wapya ni ya juu hadi inatisha
Katika mji wa Lokichar Turkana Kenya, Leah Akiru akiwa ameketi nje ya nyumba yake na watoto wake akipatiwa mafunzo na mhudumu wa afya wa UNICEF.
UNICEF Kenya

Mradi wa NICHE umekuwa mkombozi wangu asante UNICEF: Leah Akiru

Mradi unaoendeshwa na serikali ya kenya  na kupigwa jeki na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambao ni wa kuboresha lishe kwa watoto kwa kugawa fedha taslim na elimu ya afya au NICHE (NISHI) umeleta nuru kwa wakazi wa Lokichar katika kaunti ya Turkana Kaskazini Mashariki mwa Kenya na miongoni mwa wanufaika ni Leah Akiru.

Sauti
2'20"
Mkunga anayefanya kazi katika kliniki tembezi ya afya inayoungwa mkono na UNFPA akimkabidhi Francine binti yake mchanga, Amani.
© UNFPA DRC/Jonas Yunus

Nitamuita mtoto wangu Amani kwasababu amezaliwa katika vita, DRC

Wakati mapigano yalipozidi kushika kasi katika Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC), Francine Toyata alishikilia tumbo lake la ujauzito, maumivu yakimshika kwa wimbi la uchungu. Ilikuwa saa 2 asubuhi wakati alipoanza kusikia uchungu wa kujifungua, katikati ya eneo la vita. "Nimehamishwa mara mbili tangu Januari, na nilikuwa nikijificha katika kambi iliyojaa watu kupita kiasi," ameliambia shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ya Uzazi na Idadi ya Watu (UNFPA).

Makazi ya wakimbizi wa ndani ya Lushagala Kivu Kaskazini nchini DRC. (Maktaba)
© UNHCR/Guerchom Ndebo

DRC: Mashambulizi yakishamiri, sinfohamu yakumba wakimbizi

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, lina wasiwasi mkubwa kuhusu janga la kibinadamu linalozidi kuwa baya tena kwa kasi kubwa huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kwani kushindwa kufikia wahitaji kumekwamisha ufikishaji misaada ya haraka inahoyitajika.

Sauti
2'37"