Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Masuala ya UM

Udugu wa Kibinadamu
OHCHR

Tutafute majadiliano badala ya kugawanyika - Katibu Mkuu UN

Ikiwa kesho Februari 4 ni Siku ya Kimataifa ya Udugu wa Kibinadamu, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres,kupitia ujumbe mahususi kwa ajili ya siku hii ametoa wito wa kuimarisha umoja, usawa, na kuheshimiana katika kipindi hiki cha ongezeko la ubaguzi na kutovumiliana duniani. Anold Kayanda na maelezo zaidi.

Hospitali ya Kamal Adwan kaskazini mwa Gaza imeharibiwa katika mzozo huo.
© WHO video

Raia wa Gaza wanatutegemea sisi ili kuendelea kuishi: UNRWA

Shirika kubwa zaidi la Umoja wa Mataifa la msaada kwa wakimbizi wa Kipalestina katika eneo linalokaliwa kwa mabavu  UNRWA, leo limesema kwamba wafanyakazi wake bado wanaendelea kutoa misaada ya kibinadamu kwa watu wa Gaza na Ukingo wa Magharibi, ikiwemo Jerusalem Mashariki, ambao wanawategemea shirika hilo ili waendelee kuishi.

Katibu Mkuu wa UN António Guterres akihutubia Jukwaa la Kiuchumi duniani, WEF huko Davos, Uswisi Jumatano 22 Januari 2025
UN/Stéphane Dujarric

Ukosefu wa ushirikiano wa kimataifa unaiweka dunia rehani kwa majanga ya mabadiliko ya tabianchi na AI: Guterres

Viongozi wa kimataifa wa masuala ya kisiasa na biashara wanaokutana Davos Uswisi kwa ajili ya jukwaa la kiuchumi duniani WEF, leo wamekabiliwa na ukweli mchungu kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, akilaani ukosefu wa ushirikiano wa kimataifa katika dunia inayokosa mwelekeo, ikikabiliwa na hatari mbili kubwa ambazo ni mabadiliko ya tabianchi na akili mnemba au AI isiyodhibitiwa. 

Sauti
3'20"
Wazima moto wakikabiliana na moto wa nyika katika eneo la Palisades karibu na jiji la Marekani la Los Angeles huko California.
© CAL FIRE

MUHTASARI: MAREKANI/TABIANCHI/WHO/GAZA

  1. Kauli ya UN baada ya Marekani kujitoa mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi
  2. WHO nayo yasikitishwa na Rais Donald Trump kuiondoa Marekani kwenye shirika hilo
  3. Harakati za wananchi wa Gaza kurejea nyumbani na kauli ya UNRWA