Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Siku za UN

Bango la siku ya Lugha mama
UNESCO

Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Lugha Mama yatimiza robo karne

Maadhimisho haya yam waka huu ya Siku ya Kimataifa ya Lugha Mama yanaangazia robo karne ya juhudi za kujitolea kuhifadhi utofauti wa lugha na kuhimiza matumizi ya lugha za mama. Ni fursa muhimu ya kutafakari mafanikio, kurejesha ahadi, na kusisitiza jukumu muhimu la uhifadhi wa lugha katika kulinda urithi wa kitamaduni, kuboresha matokeo ya elimu, na kujenga jamii zenye amani na endelevu, linaeleza shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO).

20 FEBRUARI 2025

Hii leo jaridani mada kwa kina ikimulika harakati za uhamasishaji kabla na baada ya maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani iliyoadhimishwa hivi karibuni na mchango wa redio katika juhudi za uhifadhi wa mazingira na kuchagiza maendeleo ya jamii huko Ramogi nchini DRC. Pia tunakuletea muhtasari wa habari na uchambuzi wa maneno.

Sauti
10'37"
UN News

Redio imetusaidia kufikisha elimu kwa umma kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi

Ikiwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, makala inatupeleka jijini Nairobi, Kenya ambako ambako Kevin Keitany wa redio washirika wetu Domus FM kwa kuzingatia kuwa kesho Februari 13 ni Siku ya Kimataifa ya Redio, ametutumia maoni ya vijana wawili wanaozungumzia namna redio imewasaidia kusambaza ujumbe wao kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
3'12"
Mwanamke mmoja mjini Kigali, Rwanda, ameajiriwa katika kiwanda baada ya kusomea uhandisi.
© UN Women/Geno Ochieng

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN katika Siku ya Kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi

Miaka kumi iliyopita, maadhimisho ya kwanza ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi yalitambua ukweli wa kimsingi; ushiriki wa wanawake ni muhimu kwa ajili ya kujenga ulimwengu bora kupitia sayansi na teknolojia. Nilijionea uwezo huo mkubwa nilipokuwa nikifundisha uhandisi, na niliona talanta ya ajabu, ubunifu, na azimio la wanasayansi wengi wa kike, anasema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres katika ujumbe  wake mahususi kwa ajili ya siku hii ambayo mwaka huu wa 2025 imetimiza muongo mmoja.