Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Msaada wa Kibinadamu

Wanaume wawili wakishikilia makazi ya hema huku msimu wa hewa ya baridi ukiendelea huko Gaza.
UN News

Watoto watota kwa mvua Gaza, huku baridi kali ikitishia afya zao

Huko Gaza Kaskazini, kwenye eneo la wapalestina linalokaliwa na Israeli, wanafamilia zilizofurushwa makwao kutokana na vita kati ya Israeli na wanamgambo wa Hamas wanavumilia msimu wa baridi kali katika makazi ya muda ya mahema yanayopigwa na upepo na mvua usiku na mchana, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF. Nyumba zao zimeharibika na kuacha watoto kuishi katika mazingira mabaya. 

Sauti
2'18"
Wanawake mjini Goma, jimboni Kivu Kaskazini wakibeba chakula kilichowasilishwa na  Umoja wa Mataifa na wadau wake.
WFP

WFP yatahadharisha kuhusu tishio la njaa Mashariki mwa DRC  huku watu zaidi wakizikimbia kambi

Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani WFP, limerejelea kwa kiasi usambazaji wa misaada ya chakula katika sehemu za Goma, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), likitoa msaada muhimu wa lishe kwa wastani wa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miezi 59 waliokumbwa na utapiamlo, huku mapigano ya wiki tatu yakizidi kuathiri vibaya upatikanaji wa chakula kwa wale walio hatarini.

Mtoto akibeba maji kupitia eneo la kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kanyaruchinya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNICEF/Arlette Bashizi

Watoto wa DRC wanakabiliwa na ukiukwaji mkubwa wa haki, yaonya Kamati ya UN ya Haki za Mtoto

Watoto katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wanakabiliwa na janga lisilo na kifani, wakivumilia ukiukwaji mkubwa wa haki zao, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kiholela, ukatili wa kingono, uandikishaji wa kulazimishwa na utekaji nyara unaofanywa na pande zinazohusika katika mzozo, Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Mtoto imeonya leo jijini Geneva, Uswisi.

Ndege isiyokuwa na rubani au drone ikijiandaa kupaa huko Goma, Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo -DRC. (Maktaba)
UN Photo/Sylvain Liechti

Mzozo DRC: OCHA yasihi kufunguliwa kwa viwanja vya ndege Goma na Kavumu

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likifanya kikao cha dharura jijini New York, Marekani kujadili hali ya usalama inayozidi kuzorota kila uchao huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa Masuala ya kibinadamu nchini humo, Bruno Lemarquis amesema kupanuka kwa mzozo huo kumezidi kugharimu maisha na mustakabali wa raia.

Sauti
1'55"