Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Haki za binadamu

Patrice Vahard, Mkurugenzi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Pamoja ya Haki za Binadamu, UNJHRO, nchini DRC, akiwa ziarani Beni, Kivu Kaskazini.
BCNUDH RDC

DRC: Majaji, mawakili mafichoni baada ya wafungwa kutoroka jela Goma, raia nao mashakani

Wakati waasi wa M23 ikiendelea kusonga mbele kuelekea ‘maeneo mengine ya kimkakati’ mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, baada ya kuteka miji ya Goma jimboni Kivu Kaskazini na Bukavu na Kamanyola jimboni Kivu Kusini Umoja Mataifa umeelezea wasiwasi wake kuhusu athari mbaya za kutoroka kwa wafungwa kulikoshuhudiwa Goma, pamoja na magereza makuu ya Kabare na Bukavu.

Mtoto akibeba maji kupitia eneo la kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kanyaruchinya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
© UNICEF/Arlette Bashizi

Watoto wa DRC wanakabiliwa na ukiukwaji mkubwa wa haki, yaonya Kamati ya UN ya Haki za Mtoto

Watoto katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wanakabiliwa na janga lisilo na kifani, wakivumilia ukiukwaji mkubwa wa haki zao, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kiholela, ukatili wa kingono, uandikishaji wa kulazimishwa na utekaji nyara unaofanywa na pande zinazohusika katika mzozo, Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Mtoto imeonya leo jijini Geneva, Uswisi.

Januari 2024 huko Bukavu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, watu wanaandamana kupinga kuingiliwa na mataifa ya kigeni katika uchimbaji madini na uchimbaji wa rasilimali za madini.
UN Radio Okapi

Wakiingia Bukavu, M23 wameua watoto na kukiuka haki za binadamu- OHCHR

Hali ya haki za binadamu Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, inaendelea kuzorota kwa kasi, na kusababisha ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na unyanyasaji,ukatili  kama vile watu kuuawa  kiholela, wakiwemo  watoto, na mizozo inayohusiana na  unyanyasaji wa kingono  na unyanyasaji wa kijinsia, amesema Ravina Shamdasani Msemaji wa ofisi ya Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu  OHCHR.

Watoto wakijifunza kwa kutumia kompyuta ndogo au tablet katika Shule ya Umma ya Melen ya Yaoundé, Kamerun.
© UNICEF/Frank Dejongh

Ukweli kuhusu dhana nne potofu kuhusu usalama wa mtoto mtandaoni

Maisha ya watoto na vijana kwa muda mrefu yameunganishwa na intaneti na mitandao ya kijamii na kadri teknolojia inavyoendelea kubadilika kwa kasi jambo hili linaongezeka na kuenea zaidi na kuruhusu watoto kufikia ulimwengu wa habari, kujifunza, kushirikiana, burudani na zaidi inaweza kuwa chanya lakini wakati mwingine kuna hatari, linaeleza shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF katika makala hii iliyochapishwa kwenye wavuti wa shirika hilo leo Siku ya Kimataifa ya intaneti salama.

Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu Volker Türk atembelea Hospitali ya Nitol, Bangladesh, ambapo baadhi ya wanafunzi walipiga risasi walipokuwa wakishiriki maandamano. (Maktaba)
© UNOHCHR/Anthony Headley

Bangladesh: Ripoti yabainisha ushiriki wa viongozi wa juu katika ukandamizaji

Ukandamizaji wa maandamano makubwa yaliyofanyika nchini Bangladesh mwaka jana hadi kusababisha kuangushwa kwa serikali  ya muda mrefu ya Waziri Sheikh Hasina ulisababisha vifo vya watu wapatao 1,400 ndani ya siku 46 pekee, wengi wao wakipigwa risasi na vikosi vya usalama, amesema hii leo Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu, Volker Türk, akinukuu ripoti ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, OHCHR.

Sauti
1'58"