Uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine umesababisha 'tishio la kisaikolojia', aonya mratibu mkuu wa misaada UN
Katika takriban miaka mitatu tangu uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, watu wa nchi hiyo wamevumilia mashambulizi ya mara kwa mara, “tishio la kisaikolojia, kufurushwa na mateso", ameonya Afisa wa uratibu wa misaada wa Umoja wa Mataifa nchini humo Matthias Schmale leo Ijumaa, Februari 2025.