Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Bi. Valérie Mubawa, mjasiriamali huko Goma DRC ambaye alipata mafunzo kutoka MONUSCO lakini biashara yake imeathiriwa na vurugu zinazoendelea.
UN News

Mafunzo tuliyopewa na MONUSCO na biashara zetu vimeenda mrama baada ya M23 kutwaa Goma: Mnufaika

Goma, ambao ulikuwa mji mkuu wa Jimbo la Kivu Kaskazini, Mashariki mwa DRC ulikuwa ni  kitovu cha mafunzo ya ufundi stadi ya Umoja wa Mataifa kwa wanufaika wa miradi ya kusaidia jamii kiuchumi iliyolenga wapiganaji wa zamani waliokuwa wamejiunga na makundi yenye silaha, vijana walio katika hatari na wanawake walio katika mazingira magumu.

Dkt. Kisembo Ronex Tendo kutoka Uganda ambaye ni Mkurugenzi wa shirika la Afrika Mashariki Fest.
UN News/John Kibego

Ni wakati wa kuachana na lugha za kikoloni na kukumbatia Kiswahili, Uganda tumeanza: Dkt. Kisembo

Wito wa shirika la umoja wa Mataifa la elimu  sayansi na utamaduni UNESCO wa kuinadi lugha ya Kiswahili miaka miwili iliyopita kama lugha ya kimataifa umepokelewa kwa mikono mwili na nchi mbalimbali barani Afrika na kutambua mchango wake ikiwemo Uganda itakayokuwa mwejeji wa kongamano la kimataifa la Kiswahili mwaka huu 2025 ikishirikiana na shirika la Afrika Mashariki Fest. Kwa nini Uganda imekivalia njuga Kiswahili sasa?

Fihya Al Tayeb Nasser mwenye umri wa miaka 13 ni mwanaharakati anayeoongza vuguvugu la haki za watoto kwenye jimbo la White Nile nchini Sudan.
UNICEF/UNI502078/Elfatih

Ushirikiano na harakati thabiti ni jawabu dhidi ya FGM: UNFPA, WHO, UNICEF

  • Je wajua! Leo hii wasichana na wanawake milioni 230 duniani kote ni manusura wa ukeketaji wanawake na wasichana, FGM?
  • Je wajua kuwa FGM ni ukiukaji wa haki za binadamu unaosababisha majeraha makubwa ya kimwili, kihisia na kisaikolojia kwa wasichana na wanawake.?
  • Je wajua bila hatua hivi sasa, ifikapo 2030 wanawake na wasichan milioni 27 watakuwa wanaishi wakivumilia ukiukwaji huu wa haki na utu wao ?
Jorum Nkumbi, Mmoja wa walumbi wa lugha ya Kiswahili ambaye pia ni mwandishi wa vitabu nchini Tanzania akihudhuria kongamano la Kiswahili huko Havana, Cuba.
UN News/Kiswahili

Kukumbatia lugha nyingi ni nguzo ya ujumuishwaji katika jamii: Nkumbi

Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO linasisitiza kwamba kukumbatia uwepo wa lugha mbalimbali duniani ni muhimu kwa kukuza ujumuishwaji, utofauti wa kitamaduni, na maelewano miongoni mwa watu na pia kama njia ya kuhakikisha elimu bora, kuhifadhi lugha za asili, na kuhamasisha utangamno kati ya tamaduni hasa kujifunza kwa kutumia lugha ya mama.

Kambi ya Bulengo nchini Jamhuri ya Kidekokrasia ya Congo DRC.
WFP

Sintofahamu na maombi ya wakazi wa Goma baada ya waasi wa M23 kutwaa mji huo

Malimingi, jina lake halisi limehifadhiwa kwa ajili ya usalama wake, ni mratibu wa shirika moja la kiraia la lililoko Goma, jimboni Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. Kupitia ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO, Bwana Malimingi amekuwa akifundisha vijana, wakiwemo wale waliotumikishwa vitani na kisha kujisalimisha, stadi za kutengeneza simu janja zilizoharibika, kama njia ya kujipatia kipato badala ya kutumikishwa vitani au kuingia kwenye vitendo vya kuhatarisha usalama wao.