Mzunguko mpya wa chanjo ya Polio waanza Gaza
Mzunguko wa sasa wa kampeni kubwa ya chanjo ya polio huko Gaza, inayolenga karibu watoto wachanga 600,000, imeanza Jumamosi hii ya tarehe 22 Februari 2025.
Mzunguko wa sasa wa kampeni kubwa ya chanjo ya polio huko Gaza, inayolenga karibu watoto wachanga 600,000, imeanza Jumamosi hii ya tarehe 22 Februari 2025.
Shughuli za kidiplomasia zinaongezeka muda mfupi kabla ya kutimia miaka mitatu ya uvamizi kamili wa Urusi kwa Ukraine. Ingawa hali bado ni tete, Umoja wa Mataifa unapanga jinsi bora ya kusaidia Ukraine pindi mapigano yatakapokoma.
Katika takriban miaka mitatu tangu uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine, watu wa nchi hiyo wamevumilia mashambulizi ya mara kwa mara, “tishio la kisaikolojia, kufurushwa na mateso", ameonya Afisa wa uratibu wa misaada wa Umoja wa Mataifa nchini humo Matthias Schmale leo Ijumaa, Februari 2025.
Maadhimisho haya yam waka huu ya Siku ya Kimataifa ya Lugha Mama yanaangazia robo karne ya juhudi za kujitolea kuhifadhi utofauti wa lugha na kuhimiza matumizi ya lugha za mama. Ni fursa muhimu ya kutafakari mafanikio, kurejesha ahadi, na kusisitiza jukumu muhimu la uhifadhi wa lugha katika kulinda urithi wa kitamaduni, kuboresha matokeo ya elimu, na kujenga jamii zenye amani na endelevu, linaeleza shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO).
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia wakimbizi, UNHCR limetoa ombi la dola milioni 40.4 ili kujiandaa na kutoa huduma za kuokoa maisha na usaidizi kwa wakimbizi wa ndani na waliokimbilia nchi jirani baada ya wakati huu ambapo mashambulizi ya waasi wa M23 yanazidi kufurusha raia
Huko Gaza Kaskazini, kwenye eneo la wapalestina linalokaliwa na Israeli, wanafamilia zilizofurushwa makwao kutokana na vita kati ya Israeli na wanamgambo wa Hamas wanavumilia msimu wa baridi kali katika makazi ya muda ya mahema yanayopigwa na upepo na mvua usiku na mchana, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF. Nyumba zao zimeharibika na kuacha watoto kuishi katika mazingira mabaya.
Ripoti mpya ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) iliyotolewa leo Februarai 20, 2025 inaonya kwamba uchumi wa Syria hautafikia kiwango chake cha kabla ya vita hadi mwaka 2080 kama ukuaji wa kiuchumi hautaongezeka kwa kasi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani WFP, limerejelea kwa kiasi usambazaji wa misaada ya chakula katika sehemu za Goma, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), likitoa msaada muhimu wa lishe kwa wastani wa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miezi 59 waliokumbwa na utapiamlo, huku mapigano ya wiki tatu yakizidi kuathiri vibaya upatikanaji wa chakula kwa wale walio hatarini.